Thursday, February 28, 2013

RICK ROSS AONGEZEWA ULINZI ZAIDI BAADA YA KUANDAMWA NA WAHUNI......

Rick Ross, rapper ambaye amekuwa akilengwa kushambuliwa na kundi la wahuni, ameongezewa ulinzi na polisi wa jijini New York, Marekani…. saa 24 kwasababu ya kupokea vitisho vingine.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, polisi wamekuwa wakimlinda Ross aliyefikia kwenye hoteli ya The London kwa siku za hivi karibuni. 

Vyanzo vimeuambia mtandao huo kuwa vitisho vipya dhidi ya rapper huyo mwenye makazi yake jijini Miami, Florida hajavichukulia kawaida.
Mwezi uliopita Ross akiwa anaendesha gari lake aina ya Rolls-Royce alinusurika kupigwa risasi huko Ft. Lauderdale muda mfupi baada ya kutoka kwenye party ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa. 

Hata hivyo yeye na msichana aliyekuwa naye hawakujeruhiwa.
Msaani Rick Ross akiwa jukwaani katika moja ya show zake.

No comments:

Post a Comment