Thursday, February 28, 2013

Uingereza-watakavyoishi-kifalme-brazil.

KIKOSI cha timu ya taifa ya England kimepanga kula maisha Rio de Janeiro wakati wa michuano ya Kombe la Dunia 2014, kwa kuweka kambi yake kwenye hoteli ya The Windsor Atlantica, inayojulika iliyopo kwenye fukwe za Copacabana.
 
Vijana wa Roy Hodgson wataishi kwenye hoteli hiyo ya nyota tano, ambayo iko pembezoni mwa bahari, wakati wa mechi yao ya kirafiki dhidi ya Brazil kwenye uwanja wa Maracana, Juni 2, mwaka huu.
Ndani ya Hotel hiyo.

The Windsor Atlantica yatakuwa makazi ya England, mwanzoni wa Juni.

Beach: Hoteli ya England (Jengo refu zaid) ikiangalia fukwe za Copacabana

Wamedhamiria kutumia hoteli hiyohiyo wakati wa michuano ya Kombe la Dunia, mwaka mmoja baadaye, iwapo kikosi hicho kitafuzu kushiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka 2012.
Jengo la hoteli hiyo ya nyota tano ndilo refu zaidi kwenye eneo lilipo, huku likiangalia fukwe za Copacabana ikiwa wachezaji watimu hiyo watafuzu kushiriki Kombe la Dunia.

Moja ya maeneo ya kuvuti Kaskazini mwa Havana: England watakula bata kwenye moja ya maeneo mazuri zaidi ya Rio.
Ufukwe.



 
Hoteli hiyo ina vyumba 54, huku England wakitarajiwa kuishi kwenye ghorofa ya pili nay a tatu ya hoteli hiyo, wakiwa hapo watakuwa na sehemu yao maalumu ya kula, matibabu na kujiachia.
Lakini watakutana na wananchi wengi pale watakapokatiza kwenye eneo la mapokezi la hoteli hiyo.
Haitafanana na makao makuu yao ya Kombe la Dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini ambaklo walikaa kwenye hoteli ya Royal Bafokeng Sports Campus iliyopo Rustenburg, hoteli ambayo iliwakera baadhi ya wachezaji.
Hoteli hiyo inasehemu ya spa na bafu linye shower saba kwa ajili ya kupunguza uchovu.

Sehemu ya GYM.


Kwenye michuano ya Euro mwaka jana nchini Poland, England waliweka makazi yao katikati ya mji wa Krakow.
Lakini hoteli ya Stary ilichaguliwa mahususi kwenye michuano hiyo kwa sababu za kiusalama kwa sababu kulikuwa na walinzi waliohakikisha wachezaji wanapata muda binafsi.
Wakati wakiwa hawana kazi jijini Rio, England watakuwa wakipumzika kwenye fukwe kubwa zaidi duniani za Copacabana.
Wachezaji wa England watakuwa wakila bata kwenye Bahari ya Atlantic au kwenye swimming pool ya hoteli

Windsor Atlantica pia wanatoa mataulo ya ufukweni, viti na miamvuli.
Na kwa jambo lolote ambalo England watakuwa wanataka kukabiliana nalo juu ya masuala ya Kombe la Dunia, Uongozi wa FIFA utakuwa jirani yao kwenye hoteli ya Copacabana Palace.
 

No comments:

Post a Comment