Monday, December 31, 2012

KESI YA SHEIKH PONDA YAPIGWA TENA KALENDA KUTOKANA NA MASHAHIDI KUTOFIKA MAHAKAMANI LEO.


Katibu Mkuu  wa
Jumuiya
na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda akiingia katika
chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo
pamoja na washtakiwa wenzake 49, hata hivyo kesi hiyo imeahirishwa
kutokana na mashahidi upande wa mashtaka kutofika mahakamani hapo.

Katibu Mkuu  wa  Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda akiwa na mshtakiwa mwenzake,  Mukadam Abdal Swalehe (kushoto).

Baadhi ya wafuasi wa Sheikh Ponda wakiwa katika viunga vya mahakama ya Kisutu.

Katibu Mkuu  wa  Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda na mshtakiwa mwenzake Mukadam Abdal Swalehe wakitoka mahakamani chini ya ulinzi wa askari magereza.



Ulinzi uliimarishwa katika eneo la Mahakama ya Kisutu leo.



 Katibu Mkuu  wa  Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda (kulia) akiwa na washtakiwa wenzake.

No comments:

Post a Comment