Monday, December 31, 2012

TUME YA MABADILIKO YA KATIBA, KATIKA PICHA.

NAIBU Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bw. Casmir Kyuki (kushoto) akitoa ufafanuzi kuhusu kuhusu kazi na majukumu ya kitengo cha utafiti cha Tume hiyo kwa wajumbe wa kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati walipotembelea Ofisi za Makao ya Tume hiyo jijini Dar es Salaam Oktoba 16. Wa pili kushoto ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Bi. Angellah Kairuki na Katibu wa Tume Assaa Rashid (watatukulia).

Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bw. Ismail Ngayonga akitoa ufafanuzi kuhusu kaziza Tume hiyo kwa Sarah Houlihanna Anna Lingken kutokaTaasisi ya Kisheria ya Women’s Link Worldwide ya nchini Colombia wakati walipotembelea banda la Tume hiyo katika maadhimisho ya siku ya Haki za Binadamu duniani zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali, Bw. Mohammed Mtonga (wapili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Sekretarieti ya Tumeya Mabadiliko ya Katiba, wakiongozwa na Katibu waTume, Bw. Assaa Rashid (kushoto) na Naibu Katibu, Bw. Casmir Kyuki mara baada ya kufungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wajumbe wakamati ya ukaguzi wa Tume hiyo kuhusu ukaguzi wa fedha za umma.

No comments:

Post a Comment