Tuesday, January 15, 2013

KAGASHEKI USO KWA USO NA WACHEZAJI WA SEATTLE SOUNDERS.

Waziri Balozi Kagasheki.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na ujumbe wa wachezaji na waandishi wa habari (PICHA CHINI),kutoka timu ya seattle Sounders ya Canada wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Bodi ya Utalii ya Tanzania TTB kwenye hoteli ya serena jijini Dar es salaam hapo jana. 

Kwa ajili ya ugeni huo, Bodi ya Utalii ilisaini mkataba wa kutangaza utalii wa Tanzania katika kiwanja cha timu hiyo katika ziara iliyofanywa na Waziri wa Maliasili Balozi Khamis Kagasheki nchini humo.

Katika msafara huo unaoongozwa na mchezaji wa mpira wa American Football Kevin Griffin ambaye pia ni Fan Development Marketing wa Sunders FC, wachezaji hao walitembelea mbuga za Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Mbuga ya Tarangire ambapo walipata muda wa kujionea vivutio vilivyomo katika hifadhi hizo na kupiga picha.
Waziri wa maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, uso kwa uso na timu ya SEATTLE SOUNDERS na waandishi wa habari.
                                                                      

No comments:

Post a Comment