Saturday, March 2, 2013

MAHAKAMA KUU YA ZANZIBAR KUTOA UAMUZI WA DHAMANA YA VIONGOZI WA UAMSHO TAREHE 11 MWEZI HUU.

MAHAKAMA KUU YA ZANZIBAR JANA IMEPOKEA OMBI LAKUPATIWA DHAMANA KWA VIONGOZI KUMI WA JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YAKIISLAM JUMIKI AMBAO WAKO RUMANDE KWA ZAIDI YA MIEZI MITATU SASA.

OMBI HILO LIMEWASILISHWA NA MAWAKILI WANNE WA UPANDE WA UTETEZI AMBAO NI NDUGU SALIM TAWIQ,ABDALLAH JUMA,RAJAB ABDALLAH NA SULEIMAN SALIM.

UPANDE WA SEREKALI KESI HIYO INASIMAMIWA NA MAWAKILI RAMADHANI NASIB NA RAYA MSELLEM.

OMBI HILO LIMEPOKEWA CHINI YA JAJI WA MAHAKAMA KUU ABRAHAM MWAMPASHI NAKUAHIDI KULITOLEA UAMUZI TAREHE 11 MWEZI HUU KESI HIYO ITAKAPOTAJWA TENA.

JAJI HUYO AMESEMA KUWA MAHAKAMA BAADA YAKUSKILIZA HOJA ZA PANDE ZOTE MBILI ZA MAWAKILI WA WATUHUMIWA NA SEREKALI ITATOA UAMUZI.

WASHITAKIWA WOTE KWA POMAJA WANAKABILIWA NA MASHTAKA MATATU YAKIWEMO UHARIBIFU WA MALI, KUSHAWISHI, KUCHOCHEA NA KUWARUBUNI WATU KUFANYA FUJO, HUKU MSHITAKIWA NAIBU AMIRI WA JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YAKIISLAM ZANZIBAR AZAN KHALID HAMDAN AKIKABILIWA NA MAKOSA MANNE LIKIWEMO LA UVUNJIFU WA AMANI.

TATEHE 21 MWEZI ULIOPITA JAJI MKUU WA MAHAKAMA KUU YA ZANZIBAR, ABRAHAM MWAMPASHI ALIPINGA HOJA ZA UPANDE WA MASHATAKA ZA KUTAKA KUTOKUSIKILIZWA OMBI LA UPANDE WA WATETEZI WA WASHITAKIWA KUHUSU PINGAMIZI YA DHAMANA.

No comments:

Post a Comment