Thursday, March 7, 2013

ZAO LA MUHOGO LAWA LA CHAKULA BADALA YA BIASHARA LINDI NA MTWARA.


Abdallah Nyodo akiwa amebeba mfano wa shina la muhogo likiwa na mihogo yake walilolipwa fidia y ash. 130 kupisha ujenzi wa bomba la gesi.

Kukosekana kwa soko la kuuzia zao la muhogo katika mikoa ya Lindi na Mtwara, kumeelezwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa thamani ya zao hilo.

Hali hiyo imebainika baada ya utafiti uliofanywa na shirika la Radio kwa Wakulima (FARM RADIO), kutoka jijini Arusha, linaloangalia changamoto mbali mbali wanazokabiliana nazo wakulima wa zao la muhogo katika mikoa inayolimwa kwa wingi hapa nchini.

Utafiti huo umebaini kuwa wakulima wengi wa muhogo wanatumia zao hilo kama chakula badala ya biashara kutokana na kukosa masoko ya kuuzia.

Aidha imebainika kuwa mazao ya muhogo yanapopatikana kwa wingi huishia kuharibika na kutupwa kwa kuwa hakuna masoko ya kuuzia, ambapo imefikia hatua ya baadhi ya maeneo wanaamua kutumia unga wa muhogo kama cement ya kuchanganya na udongo na hatimaye kugandikia nyumba zao.

Imeelezwa kuwa changamoto nyingi ambazo zinawakabili wakulima wa zao la muhogo ni pamoja na wakulima kukosa elimu ya namna ya huifadhi wa muhogo usishambuliwe na wadudu toka ukiwa shambani hadi unapovunwa tayari kwa kuliwa.

Changamoto nyingine ni pamoja na wakulima kutokuwa na utaalamu katika kulima zao hilo, jambo ambalo hufanya lionekane kama ni zao la asili ambalo hulimwa kwa ajili ya chakula cha asili na kwamba sio la kuwaletea kipato katika familia zao.

Baadhi ya wakulima waliohojiwa kuhusiana na zao hilo, wametoa kilio chao kikubwa kwa serikali na mashirika yanayoshughulikia kilimo kuwatafutia wataalamu wa kusaidia kulima zao hilo na kuwawezesha kupata masoko ili kuinua kipato.

No comments:

Post a Comment