Monday, March 4, 2013

Matukio mbalimbali katika Uchaguzi wa Kenya.


Wapiga kura tayari kwa foleni katika mtaa wa Kibera
Hii leo wakenya wanapiga kura katika uchaguzi wa kihistoria chini ya katiba mpya. Foleni tayari zimeanza kushuhudiwa katika vituo.
Kinyang'anyiro ni kikali kati ya Muungano wa Cord na Jubilee wa Raila Odinga na Uhuru Kenyatta.
Kwenye ukurasa huu tutakupasha matukio kila yanapojiri hadi upigaji kura utakapokamilika mwendo wa saa kumi na moja jioni.
Unaweza kututumia maoni yako kuhusu uchaguzi kwenye ukurasa wetu wa Bofya facebook

16:27 :Sehemu nyingi za starehe na ulevi mjini Nyeri Mkoa wa Kati zimefungwa na zitafunguliwa Jumanne ili kuwaruhusu wapiga kura kupiga kura. Eneo la Mkoa wa Kati lina tatizo la uraibu wa pombe
16:24: Ng'endo Angela ambaye yuko Mooa wa Kati ansema kuwa kuwa sababu ya hitilafi za kimitambo, tume imalzimika kutumia mfumo wa kawaida kwa kutumia daftari za wapiga kura. Ni Nyeri peke yake ambako shughuli hiyo ilifanikiwa kwa njia ya Elktroniki
15:54 Mwandishi wa BBC Emmanuel Igunza anasema kuwa foleni mjini Nakuru zimeanza kupungua na huenda wapiga kura wakamaliza shughuli hiyo itimiapo saa kumi na moja jioni muda wa mwisho wa kupiga kura

15:16 Mmoja wa wagombea wakuu wa urais Uhuru Kenyatta ameelezea maskitiko yake kuhusu yaliyojiri Mombasa ambako washukiwa wa kundi la MRC waliwaua polisi na raia katika mashambulizi usiku wa kuamkia leo. Lengo lao lilikuwa kuvuruga shughuli ya uchaguzi
14:57 Mwandishi wa BBC mjini Kisumu Ann Mawathe anasema milolongo ya watu imepungua sana katika sehemu nyingi za mji huo ikizingatiwa kuwa asubuhi watu walikuwa wamejaa pomoni

14:51 Kuna taarifa kuwa magari ya Abiria yameanza kuongeza nauli ya magari kwa sababu ya upungufu wa magari hayo wakati wakenya wakiwa wamejitokeza kupiga kura
Mpigaji kura mjini Mombasa
13:33 Tume ya uchaguzi imeagiza uachaguzi kurejelewa katika wodi tano kati ya zote 1'450 ambako mitambo ya tume hiyo ilikumbwa na hitilafu pamoja na makosa kwenye karatasi za kupigia kura
13:31 Katika baadhi ya vituo vya kupigia kura, ambako foleni ndefu zimeshuhudiwa, taarifa zinasema kuwa watu wanaonekana kukata tamaa na wameamua kurejea nyumbani kwani foleni hazisongi

13:24 Mwandishi wa BBC Wanyama wa Chebusire anaripoti kuwa gari la mbunge mmoja wa zamani limeteketezwa moto katika kaunti ya Kakamega na watu wanaoaminika kuwa wafuasi wa mpinzani wake.
11:25 Mkuu wa Polisi David Kimaiyo asema kuwa takriban wanachama 200 wa kundi la MRC au Mombasa Republican Council walivamia kituo cha polisi wa doria wakiwa wanaelekea kusambaratisha shughuli za kupiga kura. Inaarifiwa polisi wanne waliuawa katika makabiliano kati yao na wanachama hao.
11:14 Mgombea wa urais Uhuru Kenyatta anapiga kura yake katika eneo bunge lake la Gatundu , mkoa wa Kati

Milolongo mirefu ilishuhudiwa kote nchini
10:39 Mwandishi wa BBC aliye mjiniNyeri Ng'endo Angela anasema kila baada ya nyumba kumi kuna kituo cha kupigia kura, wapiga kura wamejitokeza kwa wingi, baadhi ya mashine za tume ya uchaguzi zilifeli lakini baada ya kushughulikiwa mambo yakarejea kuwa sawa.
10:31 Mwandishi wa BBC mjini Eldoret Wanyama wa Chebusire vituo vilifungua mapema mambo, yameenda shwari kwa ujumla wake, lakini katika baadhi ya vituo, kumekuwa na mushkil , mashine ziligoma katika kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi ya UG, zaidi ya wapiga kura elfu tatu , hadi sasa ni chini ya watu hamsini wamepiga

10:27 Mkuu wa tume huru ya uchaguzi Isaac Hassan anahutubia waandishi wa habari kuhusu changamoto inazokabiliwa nazo tume hiyo. Isaac anasema vituo vilivyofungua kuchelewa, vitahakikisha wapiga kura wote wamepiga kura

10:22: Ingawaje tume ya uchaguzi IEBC inawakubalia watu wawasindikize wazee au wagonjwa kupiga kura, wapigaji kura wengine wanawakataza kufanya hivyo. Mjini Kisumu katika kituo cha upigaji kura cha Ukumbi wa Aga Khan, mwandishi wetu Ann Mawathe dada mmoja alieyejipandikiza blanketi tumboni ili kuwahadaa watu na akubaliwe kwenda hadi mwanzo wa foleni, alikatazwa kufanya hivyo na wapiga kura wenzake.
Katika kituo hicho hicho, baba fulani aliyekuwa amebeba kipochi cha mkewe aliyekuwa na mtoto mgongoni, naye alirudishwa hadi nyuma kabisa ya foleni hiyo. Pia, mwanamume mwingine aliyejitwika ufahari fulani kwa vile alikuwa kavalia suti, na kutaka kuruka foleni, alikatazwa kufanya hivyo.

Karani katika kituo cha kupigia kura
09:04 Waziri mkuu Raila Odinga ambaye pia anagombea urais amepiga kura yake katika eneo la Kibera. Amesema licha ya kupata habari za baadhi ya vituo vya kupigia kura kuwa na hitilafu kidogo, wapiga kura wasiwe na wasiwasi kwani mambo yatakuwa shwari
08:43 Mgombea wa urais wa muungano wa CORD, waiziri mkuu Raila Odinga anatarajiwa kupiga kura yake wakati wowote kuanzia sasa

08:30 Solomon Mugera anasema kwamba kupiga kura kunachukua takriban dakika 12
08:25 Hassan Majid pia mwandishi wa BBC anasema kuwa polisi wamepata mwili mmoja wa mtu aliyeuawa na mwingine kujeruhiwa kwa kukatwa panga katika eneo la Mishomoroni

08:24 Mwandishi wa BBC mjini Mombasa, Karen Allen anasema kuwa polisi wamepata maiti za polisi wanne ambao wameuawa katika eneo la eneo la Changamwe , Kaskazini mwa Mombasa. Hana taarifa zaidi kwa sasa
Mama na mwanawe kenye kituo cha kupigia kura
08:16:Frawaso Kimutai kupitia Bofya facebook yuko katika kituo cha Menengai mjini Nakuru kura ilianza kupigwa saa moja asubuhi na foleni ni ndefu ingawa inakwenda polepole mwendo wa kobe

08:15:Fatma Sanbur yuko mtaani Kibera na anasema watu ni wengi sana lakini hakuna mbinu ya kupanga foleni. Anasema watu wanapangwa kwa orodha ya majina na hata baada ya saa moja tangu waanza kupangga foleni saa kumi na moja, shughuli ya upigaji kura ilikuwa haijaanza
07:11James Mwangi: Kwenye ukurasa wa Bofya Facebook wa Bofya bbcswahili anasema yuko kwenye foleni na habanduki
07:14 Hison Nyakundi : Yuko mjini Eldoret kwa Foleni tayari kupiga kura Bofya bbcswahili

07:24 Kips Oscar: Kupitia Bofya Facebook yuko katika kaunti ya Marsabit anasema upigaji kura unaendelea bila wasiwasi na kuwa wanatarajia shughuli itakamilika kwa muda bila wasiwasi
Usalama ulidhibitiwa asubuhi na mapema wakati upigaji kura ulipoanza
07:28: Mgombea mwenza wa Uhuru Kenyatta, William Ruro amepiga kura mjini Eldoret

07:32: William Ruto anasema kuwa anajivunia uchaguzi wa Kenya unafanyika kwa amani licha ya dukuduku la wengi. Anasema anawataka wapinzani kukubali matokeo ya uchaguzi vyovyote matokeo hayo yatakavyokuwa.
07:43 Upiga kura bado haujaanza katika baadhi ya sehemu za Kenya. Wapiga kura wanalalamika kuwa katika vituo kadhaa tarakilishi zimegoma na kwa hivyo watasubiri muda kabla ya kupiga kura zao

07:47Eco Seyar Papa akiwa mjini Nairobi anasema Wakenya wamejitokeza kwawingi jijini Nairobi katika eneo la Dagoreti. Foleni zilianza kupigwa kuanzia saa tisa usiku tangu kuanzishwa kwa demokirasia ncini Kenya watu waeneo hili hawajawai kujitokeza kwa mapenzi kama inavyo onekana.
07:50 Mwandishi wa BBC Ann Mawathe yuko mjini Kisumu na anasema ameona foleni ndefu sana watu wakiwa hamasa kupiga kura. Wamepiga foleni tangu saa nane usiku.

07:52 Mombasa eneo la Kaloleni mpiga kura mmoja amesema hadi kufikia sasa upigaji kura haujaanza kwani maafisa wa tume ya uchaguzi bado hawajawasili na vifaa vyao

No comments:

Post a Comment