Tuesday, March 5, 2013

MOURINHO NA FERGUSON WASEMA DUNIA ITASIMAMA LEO MAN UNITED NA REAL MADRID OLD TRAFFORD.

KOCHA Jose Mourinho amesema dunia itasimama leo usiku kushuhudia mpambano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Real Madrid na Manchester United. 
Kocha huyo wa Real Madrid, anaamini mchezo huo wa marudiano katika Uwanja wa Old Trafford baina ya timu hizo mbili bora Ulaya, ungekuwa fainali kwenye Uwanja wa Wembley Mei. 
Real, ambayo ilitoa sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza nyumbani Bernabeu wiki mbili zilizopita, lazima ifunge ili kuweka hai matumaini ya kwenda Robo Fainali. 
Look who's back! Mourinho has been holding court at a press conference in Manchesterconference in Manchester
Mourinho akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Manchester
Look who's back! Mourinho has been holding at a press conference in Manchester
Cristiano Ronaldo
Cristiano Ronaldo
Karibu tena Manchester: Cristiano Ronaldo akifanya mazoezi kujiandaa na mchezo wa leo usiku
City slickers: Real Madrid were put through their paces at the home of United's great rivals
Real Madrid walifanya mazoezi kwenye Uwanja wa mahasimu wakubwa wa United, Man City
Any tips? Real Madrid were put through their paces at the home of United's great rivals
Mourinho, ambaye anaonekana asiye na wasiwasi alisema: "Dunia itasimama kuangalia mechi hii. Ina mwonekano wa fainali, lakini acha tuone timu gani itakwenda Wembley. Nina shaka, matarajio yanaweza kuwa makubwa,". 
Mpinzani wake, Sir Alex Ferguson amekubaliana na hilo akisema: "Sitarajii kitu kingine kikubwa katika usiku huo Ulaya zaidi ya hiki. Klabu kubwa na historia kubwa. Huu utakuwa mchezo babu kubwa na sifikirii itakuwa ovyo,". 
Real wanajiamini na wako katika hali nzuri baada ya kuingia Fainali ya Kombe la Mfalme wiki iliyopita kwa kuwafunga mahasimu wak wakubwa, Barcelona, na pia wakashinda mechi ya ligi dhidi ya wapinzani wao hao 2-1 Uwanja wa Bernabeu. 
Not a one-man team: Former Liverpool star Xabi Alonso is another familiar face United will have to keep quiet
Nyota wa zamani wa Liverpool, Xabi Alonso ni mtu mwingine wa karibu atakayepambana na United leo
Not a one man team: Former Liverpoll man Xabi Alonso is another familiar face United will have to keep quiet
Real Madrid training
Mourinho alisema: "Nani anajua kitakachotengeneza tofauti katika mchezo - ni maswali dola milioni. Siwezi kulia ikiwa tutafungwa na nitakimbia mita 100 ikiwa tutashinda. 
"Manchester United ni wazuri kuliko walivyokuwa daima. Tayari wametwaa ubingwa wa Ligi Kuu England na ni Machi tu, hawajafungwa mechi yoyote kwa miezi kadhaa na wametinga Robo Fainali ya Kombe la FA. Nasi pia tupo katika kiwango kizuri 2013,". 
Na kwa matarajio ya Iker Casillas, ambaye amesafiri na kikosi hicho japo ni majeruhi, Mourinho ana kikosi kamili.
Mourinho alisema: "Wachezaji wana furaha. Hatuwezi kushinda ubingwa wa ligi (La Liga), lakini Ligi ya Mabingwa ni tofauti. 
Final countdown: Sir Alex and Sir Bobby Charlton watch the players train at Carrington
Sir Alex na Sir Bobby Charlton wakiwaangalia wachezaji wakifanya mazoezi Carrington
Final countdown: Sir Alex and Sir Bobby Charlton watch the players train at Carrington
Final countdown: Sir Alex and Sir Bobby Charlton watch the players train at Carrington
"Ni vizuri kucheza mechi kama hii wakati wachezaji wana furaha na wako vizuri, kwa sababu wameifunga Barcelona mara mbili.
"Tumesafiri Jumapili, kwa sababu hatukutaka kuchelewa kwenye mechi hii. Tunataka kucheza hata sasa,". 
United ina kipaumbele cha bao la ugenini baada ya mechi ya kwanza, lakini Sir Alex Ferguson anahofia kasi ya mashambulizi ya Real. 
Kocha huyo wa United, ambaye amethibitisha kwamba Ryan Giggs atacheza mechi yake ya 1,000 katika mechi ya leo, atatakiwa kupambana na nyota wake wa zamani, Cristiano Ronaldo. 
All seeing eye: Jose Mourinho kept tabs on his squad as they went through their paces
Jose Mourinho akikitazama kikosi chake mazoezini
All seeing eye: Jose Mourinho kept tabs on his squad as they went through their paces
Ferguson amesema: "Kama unajiandaa kwa mchezo unatakiwa kuheshimu uwezo wa timu nyingine, jambo ambalo tunalifanya kila wakati wa maandalizi yetu. 
"Tunafanyia kazi ubora wa timu yao, mbinu zao, nani ni wachezaji wao wazuri, na hilo tunalifanya pia kwa ajili ya Real.
"Tunatambua uimara wa timu yetu. Tunatambua nguvu yetu, tunajua tutachezaje. Ikiwa tutashinda 5-4 tutafuzu. Nafikiri kutakuwa na mabao na timu zote zitafunga. Tunapaswa kufikiria tutafunga zaidi,".
VIDEO YA MAZOEZI YA REAL MADRID UWANJA WA ETIHAD

No comments:

Post a Comment